Chui na kobe

El leopardo y la tortuga

​Kulikuwa siku moya Chui na saiba yake Kobe bakenda kupori. Chui nakamwanbia Kobe: « Saiba yangu Kobe, twende kupoli tukateke miteko. » Kobe na Chui bakenda kupoli kuteka miteko.

Bakenda kujenga nyumba yao, walipofika ku poli. Asubui, Chui akamwambia Kobe: « Saiba yangu, kila mtu aingie yake ngambo ya pori, na kila mutu ateke yake mitego. » Chui akenda yake ngambo ya pori akateka yake mitego, Kobe akenda ngambo ya poli, akateka yake miteko.

Tiii, usiku unakucha, Chui akasema: « Twende tukangalie mitego. » Chui akaenda kwake akaleta nyama. Kobe akaenda kwake akaleta uyoga. Chui akasema: « Mwenzangu, uliteka miteko unaleta tu buyoka! Mie naleta nyama ku mitego yenyewe mie niliteka: miteko gani ile unatekaka?

Kiisha kupika kila mtu chakula yake, Chui akasema: « Twende tukaoke. » Walipofika kule ku muto, Chui akaingia wa kwanza ku mayi, lakini akatoka wepesi kwani hakuwa anajuwa kuogelea mzuli. Kobe akamwambia: « Wewe haujui kuoka weye! Uniangalie mie. » Kobe akaingia mu mayi, akenda tii, anakuwa mbali na mwenzake, akavuka inchi kavu, akaenda na uficho mpaka ku dombe yao. Akakula nyama yote ya Chui. Kiisha, tumbu tele, akarudia tena, anaingia mu mayi, anakuya kutokea kwenyewe Chui alikuwa. Anamwambia: « Mwenjangu, wewe haujui kuogelea, unaona vile mimi naogelea. Wewe haugawiyake ku mayi. »

Bakarudia ku dombe yao. Walipofika, Chui akaenda kuangalia chungu yake ya nyama. Hakukuta tena kitu. Akalalamika: « Aah! Kobe nani anakula nyama hivi? » Kobe akasema: « Akose ni benyewe balitoka ku mugini njoo balikula ile nyama. Uikale tu si neno. » Asubui, Chui akenda kumiteko, akaleta tena nyama. Kobe akenda ku yake, akaleta tu buyoka.

Chui akasema: « Twende tukaoke nduku yangu. » Bakenda kuoka. Chui akaogelea, akaogelea, akavuka. Kobe akamwambia: « Mimi nikuoneshe kwenyewe banaogeleaka. » Kobe akaingia, akaenda kutokea mbali, akaya kufika tena pale ku dombe yao. Akakula nyama, akarudia. « Mwenzangu unaona kwenyewe banaogeleaka. » Chui akashangaa.

Tiii, bakarudi ku dombe yao. Kufika tena kule, Chui akakuta nyama inalika kwake ku nyumba. Chui akasema: « Mie nitaangalia mwenyewe iko ananifanya hii mayele. » Siku ingine, kiisha kupika chakula yao, Chui akamwambia Kobe: « Twende tukaoke ku muto. »

Ku njia, Chui akasema: « Kobe, mimi nabakia kwanza ku choo. » Akaya tii, akaya kukamata udongo, akatengeneza sanamu ya mutu, akaipakala ulimbu, akaiweka karibu ya chungu yake ya nyama. Akarudi akamfwata mwenzake. Chui alipofika, akaogelea, akaogelea, akavuka.

Kobe akasema: « Mie ningali naogelea kwanza. » Kobe akaingia ndani ya mayi, akavuka kwenyewe anavukaka, akenda mpaka ku dombe, kufika kule, anakula nyama, anakula nyama, anatwala saani ampatia ile udongo yenyewe. Chui alitengeneza sura ya mutu. Kobe akasema: « Kula mbio. Chui asiye kutukuta tuko tunakula nyama yake. » Akamwambia tena: « Kule mbio, kule mbio, Chui asiye kutukuta tuko tunakula nyama yake. Wewe haupende kula nyama? Kula, mwenyewe nyama anataka kuya sasa hivi. »

Hivi alikuwa anamunyamazia, Kobe akambamba kofi, mkono ukakamata ku ile sanamu. Anamtupia mkulu ukakamata kule, ampike kichwa ukakakamata kule. Palepale anaambatana ku ile ulimbu. Chui kule anasema: « Aa! mwenzangu aliingia mu mayi aye? Wapi kwenyewe anapita? »

Chui akarudia ku dombe, akamukuta Kobe. Akasema: « Haann! Kumbe weye njoo unakulaka nyama yangu, Kobe! Nazaniaka mwengine mutu, kumbi ni weye. Mimi nitakuuwa leo. » Kobe akamwambia: « Rafiki, kama uko unapenda kuniuwa, unitupe juu, uniangaliake kwenyewe niko nakuya, njoo usemake: « Njoo mzee Kobe ule, njoo mzee Kobe ule. Nikajikonga ku paji lako la uso, nitakufa. »

Chui akamutupa juu. Akakuya kumwangukia Chui ku paji lake la uso, palepale Chui akafa. Njoo hivi Kobe alimdanganya Chui na akafika mpaka na kumuua.